Vita Vya Iran Vitaisha Baada ya Uchaguzi wa Novemba

Rais wa Marekani, Donald Trump, amesema anaamini vita kati ya Marekani na Iran vinaweza kumalizika muda mfupi baada ya uchaguzi wa katikati ya muhula wa Marekani unaotarajiwa kufanyika Novemba mwaka huu.

Trump amesema haamini kuwa vita hivyo vitaisha kabla ya uchaguzi huo, akidai kuwa Iran haitaweza kuendelea na mapigano kwa muda mrefu zaidi.

“Nadhani vita vitaisha mara tu baada ya uchaguzi kwa sababu hawawezi kuendelea tena,” Trump alisema Jumatano akiwa safarini kuelekea Texas, ambako alihudhuria mkutano wa chama chake cha Republican kuelekea uchaguzi huo.

Kauli hiyo imekuja wakati Trump akikabiliwa na kushuka kwa umaarufu katika baadhi ya kura za maoni, pamoja na shinikizo kutoka ndani ya chama chake la kutaka vita dhidi ya Iran vikome.

Trump pia amesema bei ya mafuta huenda ikaendelea kuwa juu hadi baada ya uchaguzi, akitabiri kuwa itashuka kwa kasi baada ya uchaguzi huo.

“Mara tu baada ya uchaguzi, bei ya mafuta itaporomoka,” alisema Trump, akiongeza kuwa anaamini vita vinaweza kuchukua muda mrefu kidogo zaidi ya uchaguzi wa katikati ya muhula.

Aidha, Trump ameishutumu Iran kwa kujaribu kuathiri uchaguzi wa Marekani kwa kile alichodai kuwa ni kutaka kundi la watu “dhaifu” liingie madarakani.

Iran, kwa upande wake, imekanusha mara kwa mara madai kwamba inatafuta kutengeneza silaha za nyuklia.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii