JAMII IMETAKIWA KUJIEPUSHA NA UHALIFU MTANDAONI

Hayo yameelezwa na mtaalam mkuu wa usalama mtandaoni Yusuph Kileo alipokuwa akizungumza na  Jembe fm ambapo alipokuwa akitoa elimu ya usalama mtandaoni ikiwa dunia inaadhimisha siku ya usalama mtandaon ifikapo oktobar kila mwaka


Amesema ni kosa kisheria kusambaza taarifa ghushi mitandaoni na badala yake watumie mitandao kwa kujinufaisha katika mambo mbalimbali ambayo yatawaletea faida na hata kipato.


 Nae Hafidhi Masoud mwakilishi wa Kaimu Mkurugenzi kitengo cha ulinzi na usalama wa Tehama Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Amewasisitiza wananchi kuwa na utaratibu wa kubadili Nywila kila baada ya siku 72 na Nywila hizo zinatakiwa  kuwa madhubuti ili kuepusha kudukuliwa kwa taarifa binafsi na wametakiwa kutoa taarifa pindi watakapoona ujumbe wenye viashiria vya utapeli wa kimtandao kupitia namba 15040.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii