Rais Donald Trump amethibitisha kuwa atamkaribisha Volodymyr Zelenskiy White House Ijumaa hii kujadili msaada wa kijeshi na makombora ya Tomahawk, huku Urusi ikionya kuwa hatua hiyo ni uchokozi mkubwa dhidi yake.
Rais wa Marekani Donald Trump amethibitisha kuwa atamkaribisha Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskiy katika Ikulu ya White House siku ya Ijumaa, wiki hii. Kauli hiyo imekuja muda mfupi baada ya Zelenskiy kutangaza kuwa anasafiri kuelekea Washington kwa mazungumzo muhimu kuhusu ulinzi wa anga na uwezo wa mashambulizi ya masafa marefu wa Ukraine.
Akizungumza akiwa njiani kurejea kutoka Mashariki ya Kati, Trump alisema, "Nadhani ndiyo, tutakuwa naye hapa Ijumaa,” akithibitisha ziara hiyo itakayolenga kujadili mustakabali wa msaada wa kijeshi wa Marekani kwa Ukraine. Mazungumzo hayo yanatarajiwa kujikita katika ombi la Kyiv la kupatiwa makombora ya Tomahawk, yenye uwezo wa kufika hadi Moscow — hatua ambayo Urusi imeitaja kuwa ni uchokozi mkubwa.