WIZARA YA AFYA YAPONGEZA MAENDELEO YA MRADI UPANUZI JENGO LA MAMA NA MTOTO HOSPITALI YA RUFAA YA KANDA MKOANI MBEYA

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Seif Shekilaghe, amepongeza maendelo ya mradi wa upanuzi wa jengo la mama na mtoto na kumtaka mkandarasi kumaliza kazi iliyobakia pamoja na maboresho kabla ya tarehe 30/04/2022 ili wananchi waanze kulitumia.

Dkt.Shekhalage ameyasema leo jijini  Mbeya wakati alipotembelea Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya kujionea Hali ya utoaji huduma pamoja na kukagua maendeleo ya miradi mbalimbali inayotekelezwa na hospitali hiyo.

Katika ziara hiyo Dkt.  Shekilaghe amepokea taarifa ya hali ya utoaji huduma za afya na maendeleo ya ujenzi wa mradi wa jengo la mama na mtoto ambao kwa Sasa  umeshakamilika kwa zaidi ya asilimia 92.

Dkt. Shekilaghe, amesema kuwa Serikali kupitia Wizara ya Afya itaendelea kushirikiana na vituo vya kutolea huduma za afya nchini ili kutatua changamoto mbalimbali zilizopo kwa lengo la kuboresha hali ya utoaji huduma za matibabu kwa wananchi na kuwasihi watumishi wa afya kudumisha ushirikiano, nidhamu na maadili ya taaluma zao kazini.

Aidha, Dkt. Shekilaghe amewataka wataalamu wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya kutoa huduma kwa njia ya mkoba (outrich) ili kuwajengea uwezo watoa huduma waliopo kwenye hospitali ngazi ya mkoa na wilaya kwa ukanda wa Nyanda za juu Kusini kwa lengo la kuboresha huduma na kupunguza rufaa

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii