KUANZIA FEBRUARI WASIOCHANJWA KUTOZWA FAINI HADI TSH. 9,414,826 NCHINI AUSTRIA.

Kuanzia Februari Nchini Austria, Chanjo kwa Watu wazima itakuwa ni lazima na wote ambao hawajachanjwa watapokea wito wa kuchomwa sindano ya kwanza. Wale ambao hawatajitokeza watatozwa faini baada ya kukumbushwa


Sheria iliyowekwa inatoa hadi faini nne kwa kila Mtu ambapo Polisi watapewa uwezo wa kufanya ukaguzi kwenye Barabara Kuu. Sheria hiyo imepangwa kutumika hadi Januari 31, 2024

Serikali ya Austria inatetea hatua hii kutokana na idadi kubwa ya Wagonjwa katika Hospitali mbalimbali kutokana na maambukizi ya kirusi kipya cha ya Omicron

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii