Uwoya" Msiniige Mtaumia, Hamjui Nimepitia Msoto Gani Mpaka Kufikia Hapa".

Irene Pancras Uwoya; ni mwanamama kinara wa Bongo Movies mwenye mvuto wa kipekee nchini Tanzania ambaye anasema kuwa, huu ni wakati wake wa kufurahia mafanikio huku akiwataadharisha wanamuiga akisema; “Msiniige Mtaumia…”


Uwoya anasema kuwa, ana furaha mno na amepanga kuzunguka sehemu tofauti nchini kwa ajili ya kufurahi kwa sababu ana amani kubwa mno moyoni mwake.


Mama huyo wa mtoto mmoja anasema kuwa, amepanga akimaliza ziara ya hapa Bongo, basi ataenda kumalizia nchini Mexico ambako kuna viwanja vya bata vya kutisha.

 

“Yaani ni mwezi wa mafanikio na baraka tele kwangu, nataka kwanza nizunguke hapa Bongo nikiinjoi na nikiimaliza tu naenda zangu Mexico kwa ajili ya kumalizia raha zangu; yaani ni hivi, ni bandika bandua aisee, lakini waambie wanataka kuiga wataumi,” anasema Uwoya.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii