Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania TCRA imesema inaangalia mpango wa kuzipa kipaumbele na kuziwezesha kiuchumi runinga za mtandaoni kupitia mfuko wa Media fund ambao upo chini Wizara ya Habari.
Hayo yamesemwa na Kamati ya maudhui ya TCRA Alhamisi baada ya kukutana na waandishi wa runinga za mtandaoni katika ofisi za TCRA ikiwa ni siku chache baada ya viongozi hao kufanya ziara katika vyombo kadhaa na kujionea hali ilivyo.
Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Habbi Gunze amewataka vyombo vya habari kujikita kujenga uaminifu kwa kufanya habari kwa weledi.