Jamii imetakiwa kutambua umuhimu elimu kwa watoto wote ili waweze kupata uwezo,ujuzi na maarifa yatakayomfanya kuishi vizuri katika jamii husika
wito huo umetolewa na afisa elimu na msingi kutoka manispaa ya ilemela mwl mahero nikila bahame wakati akizungumza na jembe habari
amesema mtoto asipopelekwa shule atakosa malezi bora yanayotokana na wazazi na walimu kwasababu shule inachangia sehemu kubwa katika kumjenga mtoto kimaadili
kwa upande wake afisa maendeleo ya jamii kutoka ofisi ya mkurugenzi wa manispaa ya ilemela dawati la maendeleo ya mtoto bi sara ntangu amewataka wazazi na walezi kutowatumia watoto wao kama chanzo cha mapato bali kuwapa elimu ili iwasaidia badae .
Sasa ili kupata undani wa taarifa hii tafadhali usikose kutufuatilie na Usikilize jembe Habari Kamili hapo saa saba kamili mchana ambapo msomaji wetu wa hii leo ni Florencia Peter tafadhali usipitwe na taarifa zetu Mahiri kabisa.
Lakini pia tembelea tovuti mitandao yetu ya kijamii ya Jembefmtz
#10YrsJembefm #Familiamoja #AhsantekwaTime