CAM'RON : "Nimeingiza Takribani Bilioni 24.5 ndani ya Miaka Minne kupitia Biashara ya Dawa za Kuongeza Nguvu Za Kiume"

RAPA mkongwe kutoka Nchini Marekani ameweka wazi kuwa licha ya kwamba hayuko sana katika soko la muziki wa Hip Hop na Filamu kama ilivyokuwa mwanzo, Biashara yake ya Dawa za Kuongeza nguvu za kiume imemlipa kwa kiwango kikubwa tofauti na alivyotegemea.

Akifunguka katika moja ya interview hivi karibuni, Camron amesema kwamba Bidhaa yake hiyo ya kuongeza nguvu za kiume ambayo inafahamika kwa jina la PINK POWER HORSE, imemlipa kiasi cha USD Milioni 10 (Sawa na Tshs 24,527,213,400) ndani ya Miaka Minne.

Pia Camron amesema Mzigo huo ni asilia na Malighafi zake huwa anazitoa Nchini Senegal, ambapo huwa ni Mizizi ya Miti, Majani ya Miti, hivyo tangu ameanza biashara hiyo mpaka hivi sasa imempatia manufaa makubwa sana.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii