Rapa Fat Joe amefunguka namna ambavyo ailumizwa moyo na majibu ya msanii mwenzake Bruno
Mars baada ya "kumchenjia" mbele za watu pasipo kuangalia njia sahihi ya
kumjibu baada ya kumuuliza kama yeye ana asili ya Puerto Rico.
Akizungumza katika Podcast yake ya JOE & JADA, Fat Joe amesema kuwa,
yeye amekuwa ni shabiki mkubwa sana wa Bruno Mars kwa muda, lakini Tukio hilo
lililotokea mika 10 mpaka 15
iliyopita katika moja ya tuzo, lilimvunja moyo sana
Joe anasimulia kuwa, alikuwa ni mtu ambaye
alitamani sana kuonana Bruno Mars
baada ya kusikia kuwa yeye asili yake ni Puerto
Rico, na siku hiyo alikuwa amekaa pembeni yake. Wakati anajiandaa kuongea
naye, kuna mtu mwingine pembeni alimuonya Fat Joe kuwa asimuongeleshe Bruno Mars
suala hilo, maana ni Mtata kweli kweli, Lakini Fat Joe akaona haina ishu ,
ngoja amuulize
Katika hali ya Uchangamfu, Fat Joe alimuita Bruno
Mars na kumwambia “Yo Bruno Niaje”,
na Bruno akamjibu Fat Joe kuwa “Mambo
Vipi Joe?”. Fat Joe akamuuliza Bruno “Oya,
Wewe una Asili ya Puerto Rico?” lakini Bruno alimjibu “Unazungumza Upuuzi Gani?, Mimi ni Raia Wa Puerto Rico?, usithubutu
kuniuliza tena swali la kipuuzi kama hilo maishani Mwako”
Fat Joe anaongeza kuwa , Kauli hiyo ilimuuma na
kumvunja moyo sana maana alipayuka kwa nguvu sana