Baraza la madiwani kumfukuza mfanyakazi mtoro


Baraza la madiwani la halmashauri ya wilaya ya Mbinga limeazimia kumfukuza kazi mfanyakazi mmoja wa halmashauri hiyo kwa kosa la utoro kazini huku likiwapeleka kwenye kamati ya maadili wafanyakazi watatu wa halmashauri hiyo wakiwa na makosa hayo hayo ya utoro katika vituo vyao vya kazi.

Akisoma maamuzi ya baraza hilo Desdeurius Haule, ambaye ni Mwenyekiti wa halmashauri hiyo amesema baraza limeazimia kumfukuza kazi mfanyakazi mmoja pia limewapeleka katika kamati ya maadili wafanyakazi watatu wa halmashauri hiyo kwa makosa hayo hayo ya utoro katika vituo vyao vya kazi.


Aidha, Haule amesema kabla ya kuwajadili wafanyakazi hao walifanya jitihada kubwa ya kuwatafuta na kuwaandikia barua lakini wafanyakazi hao wameonekana hawako tayari kufanya kazi katika maeneo hayo

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii