Wanasayansi kutengeneza mtoto kwenye maabara

Wanasayansi wanaendelea kutafiti kisayansi kuhusu njia mpya ya uzazi itakayotumika kutengeneza mtoto maabara bila kufuata njia za kawaida za uzazi zinazohusisha ubebaji wa mimba na kuzaa.
Njia hii inaenda mbali zaidi, kuliko inayotumika sasa, ambayo mwanamke anaweza kupandikizwa mbegu na kuzaa bila kujamiiana.
Wanasayansi hao wanachokifanya sasa ni kutengeneza mfuko wa uzazi wa binadamu nje ya tumbo lake lengo ni kufanya mfumo huweze kubeba na kutunza mtoto sawa na mfumo wa mwanadamu.
Majaribio ya utafiti huo yamefanyika kwa kutumia kondoo na kufanikiwa.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii