Wanajeshi wa Mali wauawa na wapiganaji wa jihadi

Wanajeshi wawili wa Mali wameuawa katika shambulizi linalodaiwa kufanywa na wapiganaji wa jihadi.

Shambulio hilo limetokea kwenye kituo cha Niafunké katikati mwa Mali Jumapili asubuhi.

Watano kati ya wanamgambo hao wameuawa wakati wa shambulio hilo.

Jeshi la Mali, ambalo limekuwa likihangaika kuwadhibiti waasi wa kijihadi, limekuwa likiendesha operesheni ya kuharibu kambi za wanajihadi.

Rais wa zamani Ibrahim Boubacar Keita alitimuliwa na jeshi mnamo mwaka 2020 baada ya kushutumiwa kwa kushindwa katika vita dhidi ya uasi.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii