Akitoa taarifa kwa niaba ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilemela, Mratibu wa TASAF Manispaa ya Ilemela, Leonard Robert amesema katika awamu ya tatu ya TASAF, halmashauri ya manispaa ya Ilemela imetoa ruzuku ya zaidi ya Sh bilioni sita kuanzia mwaka 2020 hadi sasa kwa kaya maskini zaidi ya 5000.
Kwa upande wa miradi ya kupunguza umaskini, amesema halmashauri ilipokea zaidi ya Sh bilioni 2.9 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi 46 ya maendeleo.
Makamu Mkuu wa Shule ya Sekondari Igogwe Uswege Mwakalobo amesema gharama za ujenzi wa shule hiyo zimetona na TASAF kwa kushirikiana na jamii inayoizunguka shule hiyo ikiwemo michango yao ya kushiriki kwenye ujenzi.
Aidha amesema TASAF imefadhili jumla ya miradi 12 iliyotekelezwa katika shule ambayo imegharimu kiasi cha Sh milioni 891 na ameitaja baadhi ya miradi hiyo kuwa ni pamoja na ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa na vyoo sita uliogharimu Sh milioni 67.3 ujenzi wa jengo la utawala hatua ya awali ya kuezeka Sh milioni 48.7, ujenzi wa paa hadi hatua ya kukamilika ambapo Sh milioni 72.44 na ujenzi wa maabara ambapo kiasi cha Sh milioni 68.3 kilitumika.