TUNDU LISSU AIOMBA MAHAKAMA KUJITETEA

Mwenyekiti ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Tundu Lissu ameiomba Mahakama kupewa nafasi ya kujitetee mwenyewe huku akitaja sababu ni kuwa mawakili wake kutopewa nafasi ya faragha kuzungumza naye Gerezani.

Lissu amebainisha hayo leo Jumatatu Juni 16, 2025 wakati kesi yake ikianza kusikilizwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Jiji  Dar es salaam huku hali ya ulinzi  wa polisi  umeimarishwa katika Mahakama hiyo

Awali katika chumba cha Mahakama, Askofu Emmaus Mwamakula alimtambulisha mmoja wa watu ambaye amesema anapaswa kuiombea kesi hiyo kabla ya kuanza

Aidha Wananchi  na viongozi mbalimbali  wa Chadema waliokuwepo kwenye chumba cha mahakama walisimama na wengine kufumba macho kushiriki maombi hayo

Ikumbukwe Mhe Lisu anakabiliwa na kesi mbili tofauti kesi ya uhaini pamoja na kesi  kuchapisha taarifa za uwongo mtandaoni.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii