Ndege ya Air India Boeing 787 Dreamliner iliyokuwa safarini kutoka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Sardar Vallabhbhai Patel, Ahmedabad, kuelekea London, imeanguka muda mfupi baada ya kuruka mchana wa leo Alhamisi, tarehe 12 Juni 2025.
Ndege AI 171 iliruka saa 7:38 mchana (IST), lakini baada ya takriban dakika tano, ilishuka kwa kasi na kuanguka katika eneo la makazi la Meghani Nagar, karibu na uwanja wa ndege.
Ajali hiyo ilisababisha mlipuko mkubwa na moshi mzito mweusi, uliosababisha hofu kubwa miongoni mwa wakazi.
Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii