Uamuzi wa ICJ kutoa uamuzi wake kuhusu malalamiko ya Khartoum dhidi ya UAE

Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ) iko tayari kutoa uamuzi wake kuhusu malalamiko ya Sudani dhidi ya Falme za Kiarabu Mei 5, 2025. Khartoum imeishtaki UAE mbele ya Mahakama ya Kimataifa ya Haki ya Hague, Uholanzi, ikiishutumu kuhusika na mauaji ya kimbari dhidi ya watu kutoka jamii ya Masalit, kutokana na madai yake ya kuunga mkono Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF) ambavyo vinapigana kwa miaka miwili na Jeshi la Sudani.

Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ) mjini Hague inatakiwa kutoa uamuzi wake tarehe 5 Mei 2025 kuhusu ombi lililowasilishwa na Sudani dhidi ya Falme za Kiarabu. Khartoum inawatuhumu kuwa "injini" ya "mauaji ya halaiki" yanayoendelea dhidi ya wakazi wa Darfur, kwa sababu ya madai yao ya kuunga mkono Vikosi vya Msaada wa Haraka vya Jenerali Hemedti (RSF).

Khartoum inatarajia maamuzi mawili kutoka kwa majaji: kwamba wanaamuru UAE kusitisha madai yake ya kuunga mkono RSF, na kwamba wanaitaka ilipe "fidia" kwa wahasiriwa wa mzozo huo.

Ripoti kadhaa za mashirika yasiyo ya kiserikali na wataalam wa Umoja wa Mataifa zimeelezea msaada wa Falme za Kiarabu kwa RSF, hasa kupitia utoaji wa silaha. Lakini Imarati inakanusha kuhusika katika mzozo huu. Wakati wa vikao mwezi Aprili, walikashifu madai "ya kubuni" na wametoa taarifa nyingi katika siku za hivi karibuni wakiishutumu Sudani kwa kuishawishi mahakama.

Inachotumaini Imarati zaidi ni kwamba ICJ itatangaza kuwa haina uwezo kwa kesi hii. Kwa sababu walipotia saini Mkataba wa Kuzuia Uhalifu wa Mauaji ya Kimbari wa mwaka 1948, waliweka nafasi, ambayo inaweka mipaka kwa nchi nyingine kuwashambulia. Je, kujizuia huku kutatumika au hakutatumika katika kesi hii? Hii ndio hoja nzima ya uamuzi wa leo Jumatatu.

Hata kama ICJ inakosa uwezo wa kutekeleza maamuzi yake, vikwazo vitaiweka hatarini UAE, ambayo ina maslahi makubwa ya kiuchumi nchini Sudani. Kulingana na vyanzo kadhaa, sehemu kubwa ya dhahabu inayochimbwa huko Darfur inasafirishwa kwenda Abu Dhabi.

Vita ambavyo vimekuwa vikiendelea tangu Aprili 15, 2023 kati ya jeshi la serikali, linaloongozwa na Abdel Fattah Abdelrahman Burhan, na RSF, inayoongozwa na makamu wake wa zamani Mohamed Hamdane Daglo, anayejulikana kama "Hemedti," vimesababisha makumi ya maelfu ya watu kuuawa nchini Sudani, kuwahamisha watu milioni 13 na kutumbukiza baadhi ya maeneo katika janga la njaa, na kusababisha janga kubwa la kibinadamu duniani, kulingana na Umoja wa Mataifa.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii