Watakao wazuia Wanafunzi kwenda shule kukiona: Serikali

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amesema Serikali itamchukulia hatua mzazi au mtu yeyote atakayemzuia mwanafunzi kupata haki yake ya elimu, na kuwataka wazazi wote wenye wanafunzi waliofaulu kujiunga na kidato cha kwanza, kuhakikisha watoto hao wanaripoti kwenye shule walizopangiwa mara moja.

Majaliwa ameyasema hayo hii leo Februari 10, 2023 wakati akiahirisha Mkutano wa 10 wa Bunge la 12, Bungeni Jijini Dodoma na kutumia fursa hio kuziagiza Mamlaka za Serikali za Mitaa ambazo bado hazijakamilisha ujenzi wa vyumba vya madarasa kuhakikisha vyumba hivyo vinakamilika.

Amesema, katika mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali ilitoa shilingi bilioni 160 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba 8,000 vya madarasa katika shule za sekondari ikiwa ni maandalizi ya kupokea wanafunzi wote waliofaulu kujiunga na kidato cha kwanza mwaka 2023.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii