Jeshi la Polisi mkoani Mbeya, linamshikilia Mwalimu Elisha Chonya kwa tuhuma za kuwakalisha chini wanafunzi wa kidato cha kwanza Shule ya Sekondari Sinde na kisha kuwapiga picha na kusambaza kwenye mitandao ya kijamii akimainisha kuwa kuna uhaba wa madawati.
Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama, ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Beno Malisa amethibitisha kutokea kwa tukio hilo mbele ya Waandishi wa Habari na kusema mtuhumiwa alikuwa mwalimu wa mafunzo ya vitendo na sio mwajiriwa.
Amesema, “Taarifa zilisambaa kwenye mitandao ya kijamii zikionyesha wanafunzi wakiwa wamekaa chini kwenye chumba kimoja cha darasa kwa madai ya uhaba wa madawati sio za kweli ni uzushi na kuwataka wananchi kuzipuuza kutokana na kuzua taharuki.”