CHONGOLA AWAONYA MAKADA WANAOKUA NA FITINA KWA WAGOMBEA

Katibu Mkuu wa CCM, Daniel Chongolo, amewaonya viongozi waliopewa dhamana na chama hicho, kuacha kueneza fitina na majungu dhidi ya wengine wakati wa uchaguzi wa ndani.

Chongolo ameyasema hayo leo Mei 27, 2022 wakati akisalimia wanachama wa CCM Mkoa wa Shinyanga, alipofika kwa ajili ya ziara ya kikazi.

Mtendaji Mkuu huyo wa CCM, amesema chama hicho kina utaratibu, Katiba, Kanuni na miongozo iliyondaliwa vizuri.

Amewataka kutenda haki, akieleza kuwa haiwezekani wakati wote tangu mwaka 2017 viongozi hao wamekuwa ndani ya CCM lakini hawakuwahi kuonywa wala kujadiliwa kwenye vikao vya maadili, iweje tuhuma hizo ziibuke sasa.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii