Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky amewasiliana na Umoja wa Afrika (AU) ili kuunga mkono uvamizi wa Urusi na kuomba kulihutubia shirika la bara hilo.
Bw Zelensky alimpigia simu Rais wa Senegal Macky Sall siku ya Jumatatu na mazungumzo yao yaligusia taarifa ya AU mwezi Februari iliyotaka kusitishwa mara moja kwa mapigano na kurejelewa kwa mazungumzo.
Mataifa ya Afrika yameonyesha kutokuwa na umoja katika kukabiliana na uvamizi wa Urusi nchini Ukraine.
Senegal ilikuwa miongoni mwa nchi 17 za Kiafrika ambazo hazikupiga kura katika Umoja wa Mataifa kuhusu azimio la kutaka Urusi ikomeshe operesheni yake ya kijeshi nchini Ukraine.
Katika mazungumzo hayo ya simu, Bw Zelensky alimfahamisha Bw Sall kuhusu "mapambano ya Ukraine dhidi ya uvamizi na uhalifu wa kutisha wa mchokozi wa Urusi", kulingana na ujumbe wa Twitter.
Bw Sall, rais wa sasa wa AU, alithibitisha mazungumzo hayo na ombi la Bw Zelensky kuhutubia Umoja wa Afrika.