Watahiniwa Mapacha Wavunja Rekodi.

Familia moja jijini Nairobi inasherehekea baada ya watoto wao mapacha ambao hawajawahi kufungamana darasani kuvunja rekodi katika Mtihani wa Kitaifa wa Darasa la Nane(KCPE).
Pacha hao wasiofanana, Bett Lindsey Kiprotich na Bett Lee Kiprotich walipata alama 414 wakiibuka miongoni mwa watahiniwa waliofanya vyema nchini.
Wawili hao waliwekewa mwanya wa 14 pekee na Magata Bruce Makenzi wa Gilgil Hills Academy, ambaye ndiye alikuwa mwanafunzi bora nchini.
Matokeo ya mapacha hao yalivuta hisia za wengi kwani hawajawahi kufungamana darasani isipokuwa somo la Hisabati, jambo la kushangaza likiwa walipata alama sawa katika mtihani wa taifa.
Wote wawili walikuwa wanasomea katika Shule ya Mountain View jijini Nairobi ambayo pia iliandikisha matokeo bora ya KCPE.
"Wakati mwingine, angepata 380 na mimi ningepata 410, mara ya kwanza inafanyika," Lindsey alisema.
"Tungefunga tu katika Hisabati ambapo sote tungepata asilimia 100 au 95," aliongeza.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii