Mwanamke Mwenye Kucha Ndefu Zaidi Duniani Hatimaye Azikata kwa Mara ya Kwanza

Ayanna Williams, mwanamke anayeishi Texas ambaye alishikilia rekodi ya 'Guinness World Record ya kuwa na kucha ndefu zaidi duniani, hatimaye amezikata baada ya miaka 30.
Lakini kulingana na Guinness World Record, alivunja rekodi yake ya kwanza baada ya kucha zake kuwa na futi 24 kabla ya kuzikata siku ya wikendi Aprili 7, 2021.


Williams aliweka rekodi hiyo mwaka 2017 ambapo kucha zake zilikuwa zina futi 18 na alikuwa anatumia chupa mbili za rangi kuzirembesha.
"Nimekuwa nikizifuga kucha zangu kwa miongo kadhaa sasa. Niko tayari kwa maisha mapya. Najua nitazikosa sana lakini wakati wa kuzitoa umefika."

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii