Mkuu wa CIA Afanya Ziara ya Siri Moscow, Putin Apewa Onyo Kali

Mkurugenzi wa Shirika la Ujasusi la Marekani (CIA), John Ratcliffe, ameripotiwa kufanya ziara ya siri mjini Moscow kwa kutumia ndege ya kijeshi ya Marekani, huku akikutana na viongozi wakuu wa ujasusi wa Urusi.

Kwa mujibu wa taarifa zilizoripotiwa na The Wall Street Journal na The New York Times, Ratcliffe alipeleka ujumbe mzito kwa Moscow kuhusu vita vya Ukraine na mahusiano ya Urusi na NATO.

Inadaiwa kuwa katika mazungumzo hayo, Ratcliffe aliionya Urusi kutoshambulia nchi wanachama wa NATO, huku taarifa nyingine zikisema aliiambia Moscow kutathmini upya msimamo wake katika vita vya Ukraine na kutafuta makubaliano kabla hali yake ya kijeshi na kiuchumi haijawa mbaya zaidi.

Ratcliffe aliripotiwa kukutana na Aleksandr Bortnikov, mkuu wa shirika la usalama la ndani la Urusi, FSB. Rais wa Urusi, Vladimir Putin, hakukutana moja kwa moja na Ratcliffe, lakini alielezwa kuhusu mazungumzo hayo.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii