China inawasihi raia wake kuondoka Eswatini kwa sababu za kiusalama

China imewasihi raia wake kuondoka Eswatini, nchi ya kusini mwa Afrika ambayo ni moja ya mataifa machache duniani kudumisha uhusiano wa kidiplomasia na mamlaka ya Taiwani, kisiwa kinachodaiwa na Beijing, "haraka iwezekanavyo." Uamuzi huu umetangazwa rasmi kwa sababu za kiusalama.

China iliwashauri raia wake wiki hii kutosafiri kwenda Eswatini, nchi hii ndogo, yeye utawala wa kifalme mdogo wa Eswatini kwa sababu za kiusalama.

Ili kuwahimiza raia wake ambao tayari wako eneo hilo kuelekea katika nchi jirani kama vile Afrika Kusini, Wizara ya Mambo ya Nje ya China inataja "hatari zinazohusiana na usalama wa umma" na "vitendo vya uhalifu vinavyohusiana na matatizo ya ulaghai mtandaoni pamoja na michezo ya haramu ya kamari".

Eswatini inakataa "kulazimishwa"

Serikali ya Eswatini inapinga madai haya na kuyahusisha na kukamatwa kwa raia wa China mapema mwaka huu wakati wa msako wa polisi kwenye mabanda ya michezo haramu ya kamari.

Msemaji wa serikali, Thabile Mdluli, pia anaonya kuwa nchi hiyo inakataa "kulazimishwa, kuwekwa katika hali mbaya, au kuvurugiwa amani," kwa sababu ya msimamo wake wa kidiplomasia.

Kwa sababu, pamoja na Somaliland, Eswatini ni mfuasi wa mwisho wa Taiwan barani Afrika, uamuzi wa kiholela wa Mfalme Mswati III, anayetawala kama mfalme mwenye mamlaka kamil

Pamoja na Somaliland, Eswatini ndiyo nchi ya mwisho inayoiunga mkono Taiwan barani Afrika.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii