Ukraine kuunda hifadhi ya chakula cha serikali

Serikali ya Ukraine imesema itaanzisha hifadhi kubwa ya chakula cha kutosha kuwalisha watu na vikosi vya jeshi wakati huu wa uvamizi wa Urusi.Chombo cha habari cha serikali kimemnukuu Waziri Mkuu Denys Shmgal akisema serikali itakomboa nafaka na akiba zingine kwenye matumizi ya kila mwaka na nchi nzima kwa gharama ya bajeti ya serikali. Ukraine ni mzalishaji mkuu wa kimataifa wa chakula na muuzaji wa nje, lakini wachambuzi wa kilimo wamesema uvamizi wa Urusi unaweza kupunguza sana eneo lililopandwa kwa mavuno ya nafaka ya 2022, na kusababisha uhaba wa nafaka dunia. Taifa hilo limesema wakulima wataanza kupanda katika maeneo salama, lakini huenda wakakabiliwa na uhaba wa mafuta na nafaka

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii