Pipa moja la mafuta ghafi limeuzwa dola 110.34 hadi 113.67 kutegemea na eneo ambalo ununuzi huo umefanyika. Bei hiyo ni ongezeko la asilimia 0.5 hadi 1.1 kutoka kwenye bei ya masaa 24 yaliyopita.
Bei ya mafuta imeendelea kupaa
hivi leo siku ya Jumanne wakati Rais wa Marekani Donald Trump akiendelea
kutoa vitisho kwa Iran na kuapa kuchukua hatua kali ikiwa nchi hiyo itashindwa
kufungua tena Mlango-Bahari wa Hormuz, eneo ambalo ni muhimu kwa usafirishaji
wa mafuta duniani.
Pipa moja la mafuta ghafi limeuzwa dola 110.34 hadi 113.67 kutegemea na eneo
ambalo ununuzi huo umefanyika. Bei hiyo ni ongezeko la asilimia 0.5 hadi 1.1
kutoka kwenye bei ya masaa 24 yaliyopita.
Aidha vikosi vya Iran viliufunga Mlango-Bahari wa Hormuz baada ya Marekani na Israel
kuanzisha mashambulizi dhidi yao mnamo Februari 28, na kuvuruga utaratibu mzima
wa usafirishaji wa nishati hiyo.
Hata hivyo wakati bei hiyo ya mafuta ikiendelea kupaa hali bado ni ya wasiwasi na pande zote zimeendelea kushambuliana.
10YrsJembefm #Familiamoja #AhsantekwaTime