Picha za video za Reuters Television zilionyesha wazima moto wakimimina maji kwenye nyumba iliyokuwa bado inatoa moshi baada ya kushambuliwa na droni.
Mashambulizi ya droni ya Urusi yameendelea kuulenga mji wa Kharkiv kwa siku nzima, huku watu wasiopungua wawili wakijeruhiwa, akiwemo mtoto wa miaka nane.
Meya wa jiji hilo, Ihor Terekhov, amesema mashambulizi yalilenga maeneo manne tofauti, huku zaidi ya droni 20 zikiripotiwa kulipuka ndani ya jiji na kusababisha moto katika baadhi ya majengo.
Picha za Reuters zimeonyesha wazima moto wakizima moto kwenye nyumba iliyoharibiwa vibaya baada ya kushambuliwa, huku samani na sehemu za ndani zikiharibika.
Milipuko mingine iliripotiwa usiku wa manane, hali inayoonyesha mashambulizi hayo kuendelea bila kukoma.
Katika mji wa , shambulizi jingine la Urusi liliharibu jengo la makazi na biashara, ingawa hakuna majeruhi waliothibitishwa.
Wakati huo huo, ndani ya Urusi katika eneo la Belgorod Region, watu 13 wamejeruhiwa kufuatia mashambulizi ya droni kutoka Ukraine, huku mifumo ya ulinzi wa anga ikidungua droni nyingine karibu na Moscow.
10YrsJembefm #Familiamoja #AhsantekwaTime