WANAANGA wa misheni ya Artemis II wamezungumza moja kwa moja wakiwa ndani ya chombo cha anga aina ya Orion, wakielezea safari yao hadi sasa na matarajio ya hatua zinazofuata katika safari hiyo ya kihistoria.
Misheni hiyo ilizinduliwa siku ya Jumatano, ikiwa imebeba wanaanga wanne ambao wanasafiri katika safari ya takribani siku 10 kuzunguka mwezi kabla ya kurejea duniani.
Akizungumza kutoka angani, Kamanda wa misheni hiyo, Reid Wiseman, alisema walipata mtazamo wa kipekee wa Dunia kutoka angani.
Alisema waliweza kuona dunia nzima kutoka ncha hadi ncha, pamoja na mabara kama Afrika na Ulaya, na hata mwanga wa aurora (northern lights) ulioonekana kwa mbali.
10YrsJembefm #Familiamoja #AhsantekwaTime