Watu 40 wauawa katika shambulizi la droni jimboni Kordofan

Watu 40 wameuawa baada ya gari walililokuwa wamepanda wakielekea kwenye mazishi, kushambuliwa kwa droni katika eneo la Kordofan nchini Sudan.

Kwa karibu miaka mitatu, Sudani mekumbwa na vita kati ya jeshi la serikali na kikosi cha wanamgambo cha RSF, vita ambavyo vimeua maelfu ya watu na mamilioni kukimbia makazi.

Eneo la Kordofan, ambalo lina hazina kubwa ya mafuta na ardhi inayofaa kilimo linaunganisha ngome za RSF katika eneo la Darfur na mashariki mwa nchi inayodhibitiwa na jeshi la serikali.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii