Zimbabwe: Rasimu ya mageuzi ya Katiba inapanga kuongeza muhula wa rais hadi mwaka 2030

Serikali Nchini Zimbabwe siku ya Jumanne imeidhinisha  hati iliyosainiwa na Waziri wa Sheria Ziyambi Ziyambi inayoelezea mapitio makubwa ya Katiba ya Zimbabwe kupitia marekebisho ambapo miongoni mwa hatua zilizopendekezwa ni zile zilizovuja kwa vyombo vya habari, ni mabadiliko ya mfumo wa uchaguzi na upanuzi wa muhula wa rais, ambao utaimarisha mamlaka ya Emmerson Mnangagwa, ambaye alichaguliwa tena mwaka wa 2023.

Katiba ya Zimbabwe inatarajiwa kupitia mabadiliko makubwa. Serikali ya sasa inapanga mfululizo wa marekebisho yanayolenga "kuboresha utulivu wa kisiasa, kufafanua mamlaka ya kitaasisi, kuimarisha miundo ya kidemokrasia, na kukuza utulivu wa kitaifa wa muda mrefu."

Hatua kadhaa ziko kwenye ajenda, kama vile kuongeza muhula wa rais kwa miaka miwili, kutoka mitano hadi saba, hali ambayo itaongeza muhula wa sasa wa Emmerson Mnangagwa, 83, aliyechaguliwa tena mwaka wa 2023, hadi 2030. Mabadiliko mengine yaliyopendekezwa ni pamoja na mabadiliko kutoka kwa kura ya moja kwa moja ya watu wote hadi uchaguzi wa bunge na uwezekano wa rais kuteua maseneta wapya kumi, na kufanya jumla yao kufikia 90.

Kwa hivyo chama tawala cha Zanu-PF kinapanga mapitio ya katiba tangu 2013. Muswada huo, uliopendekezwa na Waziri wa Sheria Ziyambi Ziyambi na kupitishwa na serikali, sasa utajadiliwa Bungeni, ambapo chama cha rais kina wingi wa kura.

Hata hivyo upinzani ulichukua hatua haraka. Jacob Ngarivhume, kiongozi wa chama cha Transform Zimbabwe, amesema kwenye mitandao ya kijamii kwamba mabadiliko haya "yataangamiza demokrasia na kuimarisha udikteta."

#10YrsJembefm  #Familiamoja #AhsantekwaTime

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii