Simba yamtambulisha Ismael Toure

Katika kuhakikisha kikosi cha Klabu ya wekundu wa msimbazi Simba Sports  kinarejea kwenye ubora wa juu timu hiyo imemtambulisha rasmi, Ismael Toure na tayari nyota huyo  yuko nchini kwa ajili ya kukitumikia kikosi cha Wekundu wa Msimbazi.“Ni kweli tunaendelea kuboresha kikosi chetu, tumefanya mchakato huu kwa kufuata mapendekezo ya mwalimu wetu,” Ahmed All, Meneja Habari na Mawasiliano wa Simba amesema.

Sambamba na hilo jana pia  ilimtambulisha beki, Nickson Kibabage, kutoka Singida Black Stars ambapo pia  wanatajwa wako katika mazungumzo ya kiungo wake wa zamani, Clatous Chama akitokea Singida Black Stars.

Hata dirisha dogo la usajili lililotangazwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), litafungwa rasmi Januari 30, mwaka huu.

#10YrsJembefm  #Familiamoja #AhsantekwaTime

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii