Wasimamizi wa uchaguzi Tarime wahamaaishwa kuzingatia usalama wakati wa uchaguzi mkuu

Wasimamizi wa uchaguzi  mkuu 2025 wametakiwa kufanya kazi kwa kufuata  Miongozo kanuni na Sheria za uchaguzi pia Kuwa waadilifu na  kufanya kazi kwa kujiamini kwani Jeshi la Polisi Tanzania limewahakikisha ulinzi na usalama wakati wote watakapo kuwa wakitekeleza majukumu yeo.

Wito huo umetolewa na Mrakibu wa Polisi Ahmed Feruzi ambaye ni Mkuu wa Kituo cha Polisi Tarime Oktoba 26 mwaka huu wakati akizungumza na Wasimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Tarime Mji katika Ukumbi wa Sekondari ya Tarime Rorya iliyopo  MMkoni Mara.

Aidha Feruzi amewataka Wasimamizi hao kuwa mabalozi wazuri wa Amani na kuwataka kuilinda Amani ya nchi kwa maendeleo na ustawi wa taifa kwani Madhara ya Uvunjifu wa Amani ni makubwa na yanayoweza kupelekea kuzorota kwa uchumi, familia kusambaratika na wananchi kushindwa kufanya shughuli zao za kiuchumi na kijamii.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii