Kampuni ya ORYX GAS yaendelea kutoa elimu juu ya matumizi ya nishati safi

KAMPUNI ya ORYX GAS kwa kushirikiana na meneja mkuu wa mauzo na  masoko tanzania bara na visiwani Shaban Sungi wameendelea kujidhatiti na kuwafikia wananchi wa Buhongwa wilaya ya nyamagana mkoani Mwanza kwa kutoa hamasa katika matumizi ya nishati safi ya kupikia.

Akizungumza wakati wa hafla fupi ya kueendeleza kampeni ya gesi sungi amesema kuwa matumizi ya nishati chafu ya kupikia imekuwa ikisababisha vifo hasa kwa kinamama

Shabani amesema kuwa tangu kuzinduliwa kwa kampeni ya gas yente imekuwa na mwitikio mkubwa kwa wananchi kutokana na elimu wanayoitoa ya matumizi ya nishati safi ya kupikia. 

Kwa upande wake katibu tawala Wilaya ya Nyamagana  Thomas Jemes Salala ameipongeza kampuni ya ORYX  kwa kutambua uhamasishaji wa matumizi ya nishati mbadala kwa kuongeza chachu kwa serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na rais Samia Suluhu Hassan  ya matumizi ya nishati safi ya kupikia. 

Nao baadhi ya washindi wa zawadi mbalimbali kutoka kwenye kampuni ya ORYX GAS wametoa pongezi zao za dhati kwa hamasa na elimu wanayoipata   juu ya   matumizi ya nishati safi ya kupikia.


Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii