Hoteli ya kwanza ya wapenzi wa jinsia moja yafunguliwa Cuba

Waandishi wa habari walipowasili kwa ziara iliyoandaliwa na serikali katika hoteli ya kifahari katika eneo la mapumziko la Cuba la Cayo Guillermo, walilakiwa na kikundi cha densi kilichovalia nguo za kubana umbo la samaki na viatu virefu.

Juu ya mlango huo, bendera ya upinde wa mvua, ishara ya kimataifa ya wapenzi wa jinsia moja, ilipepea upepo mwanana wa Caribbean.

Hoteli ya Rainbow, iliyofafanuliwa kuwa hoteli ya kwanza ya LGBTQ ya Cuba, ilifunguliwa tena mnamo Desemba.

Wakati wageni walifurahia huduma ya nyota tano karibu na bwawa au kutembea kwenye mchanga safi, Cuba haijakuwa ikikaribisha watu wanaoshiriki mapenzi ya jinsia moja.

Katika utawala wa awali wa kiongozi wa kikomunisti Fidel Castro, wanaume na wanawake wa jinsia moja walipelekwa kwenye kambi za kazi kwa ajili ya " elimu upya."

Serikali ya Cuba na kampuni iliyo nyuma ya Hoteli hiyo, wanasema inaonesha mabadiliko.

Ubia kati ya Muthu Hotels na Gaviota, kampuni ya utalii inayoendeshwa na jeshi la Cuba, Hoteli hiyo iliwekwa kwenye orodha ya serikali ya Marekani ya mashirika yaliyowekewa vikwazo nchini Cuba hata kabla ya kuzinduliwa mnamo 2019.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii