COLONEL MUSTAPHA : "Nina Mpenzi Mpya, Ni Kiziwi "

Msanii wa Muziki wa Kizazi kipya nchini Kenya, Colonel Mustapha ameweka wazi kuwa moja kati ya vitu ambavyo anavijutia mpaka hivi sasa, ni kuwa na mahusiano ya kimapenzi na wasanii maarufu nchini humo.

Akizungumza katika mahojiano nchini humo, Colonel ambaye alifanya vema na nyimbo tofauti kama vile MTAANI.COM amesema kuwa hivi sasa yupo katika mahusiano mapya na binti mwingine ambaye hana umaarufu wowote ule na ana ulemavu wa kusikia yaani “Kiziwi”, na hatamani hata kidogo kuwa na mahusiano na mtu maarufu.

Msanii huyo ameongeza kuwa, kuwa na mahusiano na wasanii maarufu ni “Pasua Kichwa” na huwa na usumbufu mkubwa kitu ambacho kimemrudisha nyuma kimaendeleo japo hivi sasa ameanza kurudi katika ubora wake hasa kiuchumi.

Pia amebainisha kuwa, mpenzi wake wa sasa ambaye ni Kiziwi watu wengi hawamfahamu kwa sababu hajamuanika mitandaoni, ila muda ukiwadia atafanya hivyo.

Kwa mujibu wa maelezo yake, mpenzi wake huyo alipata ulemavu wa kutokusikia kutokana na ajali ya gari aliyopiata akiwa katika umri mkubwa, ajali iliyopelekea kupondwa na jiwe kichwani na kupata changamoto hiyo

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii