Waziri Ajiua Kwa Risasi Kisa Kufutwa Kazi Na Putin

Vladimirovich Starovoit, aliyekuwa Waziri wa Usafirishaji wa Urusi kati ya mwaka 2024 na 2025, amekutwa amefariki dunia kwa kile kinachoelezwa kuwa ni kujiua kwa kujipiga risasi, muda mfupi baada ya Rais Vladimir Putin kumfuta kazi.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka vyombo vya usalama vya Urusi, mwili wa Starovoit, mwenye umri wa miaka 53, ulipatikana ndani ya gari lake katika eneo la viunga vya Moscow mapema Jumatatu asubuhi. Tume ya Uchunguzi ya Shirikisho (Investigative Committee) imethibitisha tukio hilo na kusema kuwa uchunguzi wa kina unaendelea ili kubaini mazingira kamili ya kifo hicho.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii