Man City kufungua pochi kwa Echeverri

Mabingwa wa Soka Duniani, Klabu ya Manchester City wanakaribia kufikia makubaliano ya kumsajili chipukizi Claudio Echeverri kutoka River Plate ya Argentina, kwa mujibu wa 90min.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 17 amevutia baadhi ya klabu kubwa Ulaya tangu alipoingia katika kikosi cha kwanza cha River Plate mwaka wa 2023, na kucheza mara sita katika mashindano yote huku wababe hao wa Argentina wakishinda Ligi Kuu ya Argentina.

Kiungo huyo mshanbuliaji alivutia sana katika Kombe la Dunia la vijana chini ya umri wa miaka 17, akifunga hat-trick maarufu katika ushindi wa Robo Fainali dhidi ya wapinzani wao wakuu Brazil.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii