Malawi imepiga marufuku uingizaji wa mahindi kutoka Kenya na Tanzania

Kenya na Tanzania kwa muda mrefu wamekuwa vyanzo vikuu vya mahindi kwa Malawi wakati wa vipindi vya  uhaba wa chakula. Wizara ya Kilimo ya Malawi ilitangaza marufuku ya uagizaji bidhaa kutoka nje katika taarifa inayosema ugonjwa wa Mahindi unaosababishwa na Lethal Necrosis hauna tiba.

Malawi imepiga marufuku uingizaji wa mahindi kutoka Kenya na Tanzania kutokana na wasiwasi wa kuenea kwa ugonjwa wa Mahindi Lethal Necrosis ambao kunaweza kuharibu chakula kikuu kinachotegemewa huko. Zaidi ya watu milioni 4 katika nchi hiyo ya kusini mashariki mwa Afrika wanakabiliwa na uhaba wa chakula.

Kenya na Tanzania kwa muda mrefu wamekuwa vyanzo vikuu vya mahindi kwa Malawi wakati wa vipindi vya uhaba wa chakula.

Hata hivyo, Wizara ya Kilimo ya Malawi ilitangaza marufuku wiki hii ya uagizaji wa bidhaa kutoka nje katika taarifa inayosema ugonjwa wa Mahindi unaosababishwa na Lethal Necrosis hauna tiba na unaweza kusababisha hasara ya mavuno kwa asilimia 100.

Taarifa hiyo inasema Mahindi yanaweza tu kuingizwa nchini mara tu yanaposindikwa, ama kama unga au mbegu.

Henry Kamkwamba ni mtaalamu wa kilimo katika Taasisi ya Kimataifa ya Utafiti wa Sera ya Chakula. 


Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii