FIFA ilisema zabuni ya pamoja kutoka kwa Morocco, Ureno na Uhispania ndio wagombea pekee wa kuandaa mashindano hayo. FIFA walipaswa kutangaza waandaaji mwaka ujao.
Kombe la kwanza la Dunia mwaka 1930 lilifanyika nchini Uruguay na na wenyeji kushinda baada ya kuwashinda Argentina katika fainali huko Montevideo.
Uhispania imetunukiwa Kombe la Dunia wiki kadhaa baada ya mkuu wao wa zamani Luis Rubiales kulazimishwa kuachia ngazi kufuatia kumbusu mdomoni mchezaji Jenni Hermoso katika Kombe la Dunia la Wanawake.
Uamuzi huu wa Jumatano wa FIFA ni mara ya kwanza kwa Kombe la Dunia kupangwa katika mabara matatu na nchi sita, ambayo inaweza kumaanisha mechi za makundi zitalazimika kufanywa katika misimu tofauti kulingana na eneo la Dunia waliopo.