Kufuzu Kombe La Dunia 2026: Tanzania, Morocco Na Niger Kundi Moja

Timu ya Taifa ya Tanzania (TaifaStars), imepangwa Kundi E katika makundi ya kufuzu Kushiriki Michuano ya Kombe la Dunia ya mwaka 2026

Katika droo iliyochezeshwa leo makundi 9 yenye timu 6 yamepangwa, Tanzania ipo Kundi moja na timu za Taifa za Zambia, Morocco, Congo, Niger na Eritrea

Mechi za Kufuzu zitaanza Novemba 2023, na Washindi wa kila Kundi watafuzu moja kwa moja kwenda kushiriki Kombe la Dunia katika nchi za Canada, Mexico na Marekani

Timu 4 bora zilizoshika nafasi ya pili (Kutoka Makundi) zitacheza mechi za mtoano za CAF. Washindi watacheza mechi za mtoano za FIFA na timu itakayoshinda itaenda kushiriki Kombe la Dunia kama timu ya 10 kutoka Afrika

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii