Mkurugenzi mkuu wa lebo ya Next Level Music, Rayvanny amejitokeza waziwazi na kukana kuwa na akaunti yoyote kwenye mtandao wa Facebook, licha ya kuwepo na akaunti yenye jina lake na amabyo imehakikiwa na kudhibitishwa na Facebook ikiwa na wafuasi Zaidi ya milioni 2.
Kupitia instastory yake, Rayvanny alipakia picha ya skrini ambapo ukurasa huo wa Facebook unaodhaniwa kuwa wake ulikuwa unajitangaza kwamba akaunti hiyo ilikuwa sokoni tayari kuuzwa kwa mnunuzi yeyote ambaye angeafikia bei.
“Nauza huu ukurasa kwa kampuni au hata msanii yoyote anayetaka kukua kimataifa, njoo DM lakini wanunuzi wenye wako serious pekee,” Ukurasa huo uliandika.
Mtu huyo ambaye awali alidhaniwa kuwa Rayvanny hadi alizidi kusema kwamba sababu ya kuipiga mnada akaunti hiyo ni kuwa anataka kusalia kwenye mitandao mingine tu kama Instagram na Tiktok katika kile alitaja kuwa hawezi kuzi manage zote.
Vannyboy aliweka wazi kwamba huyo ni mtapeli anapetumia jina lake kwenye Facebook na kusema kuwa hana akaunti yoyote katika mtandao huo mkubwa unaomilikiwa na Meta.
Rayvanny alipakia picha ya tangazo hilo na kusema kuwa hana akaunti yoyote kwenye Facebook.
“Sina akaunti yoyote kwenye Facebook,” Rayvanny alisema