Erling Haaland aweka rekodi mpya duniani

Mshambuliaji kutoka nchini Norway na Klabu ya Manchester City Erling Haaland anaongoza katika orodha ya wachezaji wenye thamani kubwa duniani wakati wachezaji wawili wa England pekee wakiwamo kwenye 10 bora.

Nyota huyo mwenye miaka 22 amekuwa na rekodi bora katika msimu wake wa kwanza akiwa na Manchester City akifunga mabao 52.

Mchezaji huyo wa zamani wa Borussia Dortmund ameshatwaa taji la Ligi Kuu England, kabla ya kuisaidia timu yake kuifumua Manchester United mabao 2-1 katika mechi ya fainali ya Kombe la FA, kwenye Uwanja wa Wembley, wiki iliyopita.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii