Otile Brown, Meneja Noriega ‘waachana’ rasmi

Otile Brown na meneja wake Joseph Noriega wameamua rasmi kusitisha makubaliano ya kufanya kazi pamoja, ikiwa ni baada ya ushirikiano mkubwa waliokuwa nao kwa takriban miaka sita ambao unatajwa kuwa chachu ya mafanikio makubwa kwa mwimbaji huyo kutoka nchini Kenya.

Taarifa ya kutengana kwa wawili hao imechapishwa kwenye kurasa za mitandao ya kijamii za mwimbaji Otile ikithibitisha mwisho wa wawili hao kikazi licha ya mafanikio makubwa yaliyotokana na ushirikiano kati yao.

Akitoa shukrani zake kwa meneja huyo, Otile Brown amekiri jukumu muhimu ambalo Joseph Noriega alilibeba katika kazi yake, akisema kwamba Noriega alichangia kwa kiasi kikubwa ukuaji wake katika muziki.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii