Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron " Mbappe Asiondoke PSG "

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron amefichua kuwa atajaribu kumshawishi nahodha wa timu ya taifa Kylian Mbappe asiondoke katika miamba hao wa soka ya Ufaransa.

Macron alizungumza na Mbappe mwaka jana katika hali sawia na kufanikiwa kumshawishi kutia wino mkataba mpya wakati alipokuwa akiwindwa na miamba wa Uhispania Real Madrid. "Sina ufahamu tosha lakini nitajaribu na kusukuma," Macron amesema 

Taarifa zilichipuka mapema wiki hii kuwa Mbappe ameambia PSG kuwa hataongeza mkataba wake hadi mwaka 2025 na kuzua tumbo joto katika mabingwa hao wa Ligue 1. 

Mkataba wa Mbappe na PSG unakamilika mwishoni mwa msimu ujao lakini una kipengee cha kuuongeza kwa mwaka mmoja zaidi lakini Mbappe sasa hataki kipengee hicho. Iwapo kweli hatatia wino wa kuongeza mkataba, PSG wamo kwenye hatari ya kupoteza mwaka ujao bila kufaidi hata peni moja kutoka kwa uhamisho wa nyota huyo.

Hii ina maana kuwa miamba hao wa Ufaransa huenda wakalazimika kumuuza katika dirisha hili la uhamisho badala ya kusubiri hadi mwaka ujao na kutoka bwerere. Uamuzi wa Mbappe kutoongeza mkataba wake ulitangazwa kwa klabu hiyo kupitia kwa barua na taarifa hizo kutolewa na gazeti la michezo la Ufaransa L'Equipe. 

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii