"Kuhusu ujenzi wa Uwanja tuna kiwanja Kigamboni lakini pia tuna eneo ambalo lina jengo la Klabu pale Jangwani, sisi binafsi tumependelea kujenga uwanja wetu pale Jangwani na tayari taratibu zimeshaanza katika kulitekeleza hilo," alisema Hersi
Ujenzi wa uwanja ilikuwa moja ya ajenda za Injinia Hersi wakati akigombea Urais wa klabu ya Yanga
Moja ya sababu ambayo Hersi aliitaja kujenga uwanja pale Jangwani badala ya Kigamboni ambako Yanga ina eneo kubwa zaidi, ni urahisi wa kufikika kwa mashabiki
Hersi alisema wataalam waliwathibitishia kuwa katika eneo lao la uwanja wa zamani wa Kaunda, wanaweza kujenga uwanja wenye uwezo wa kuingiza mashabiki 20,000
Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii