Young yahamia Chamazi

Rasmi mchezo wa 16 Bora Kombe la Shirikisho Tanzania Barani ‘ASFC’ kati ya Mabingwa watetezi Young Africans dhidi ya Maafande wa Jeshi la Magereza Tanzania Prisons utachezwa Uwanja wa Azam Complex Chamazi.

Young Africans ambao watakuwa wenyeji wa mchezo huo utakaoanza saa moja usiku, wamethibitisha kupitia mkutano na Waandishi wa Habari uliofanyika leo Jumatano (Machi Mosi), Makao Makuu ya Klabu hiyo jijini Dar es salaam.

Afisa Habari wa Young Africans Ally Kamwe amesema mchezo huo umelazimika kupelekwa Uwanja wa Azam Complex Chamazi, kufuatia Uwanja wa Benjamin Mkapa kufungwa kwa muda, kupisha maboresho ya sehemu ya kuchezea ‘Pitch’.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii