WAZIRI MKUU WA SUDANI ABWAGA MANYANGA.

Waziri Mkuu wa Sudan, Abdallah Hamdok ametangaza kujiuzulu wadhifa huo baada ya maandamano makubwa katika mji mkuu wa nchi hiyo Khartoum, ya kupinga makubaliano ya kuongoza Serikali ya Mpito.

Hamdok amejiuzulu wadhifa huo zikiwa zimepita wiki chache tangu aliporejea madarakani, baada ya mapinduzi ya kijeshi ya mwezi Oktoba mwaka 2021.

Ametangaza uamuzi huo kupitia televisheni ya Taifa ya Sudan, huku akisema anaachia wadhifa huo ili kuruhusu mtu mwingine kusaidia Taifa hilo kuvuka katika kipindi cha mpito cha kuelekea utawala wa kidemokrasia,

Hamdok ametoa wito wa kufanyika kwa majadiliano, ili kufikiwa kwa makubaliano mapya kuhusu namna utawala mpya wa kidemokrasia utakavyoongoza Taifa hilo.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii