Robertinho aanika ramani ya Ubingwa

Kocha Mkuu Simba SC Roberto Oliveira ‘Robertinho’ amesema, ili kufanikisha ndoto za kutwaa ubingwa msimu huu 2022/23 kwa klabu hiyo, ni lazima kikosi chake kishinde michezo yote iliyosalia.

Simba SC kesho itashuka katika Dimba na Benjamin Mkapa kupapatuana na Singida Big Stars, katika mchezo wa Mzunguuko wa 22 wa Ligi Kuu Tanzania Bara.

Kocha Robertinho ametoa kauli hiyo baada ya kurejea nchini na kuanza kazi mara moja, jana Jumatano (Februari Mosi) majira ya jioni, Uwanja wa Mo Simba Arena.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii