Manzoki avunja ukimya Dar es salaam

anaipenda klabu hiyo ya Msimbazi na ataitumikia siku moja.

Manzoki amesema anajua kuna baadhi ya watu waliwahi kumuhusisha na mpango wa kusajiliwa na timu inayovaa rangi ya Kinyoka Nyoka, lakini kwake hilo halipo, kwani kama kuna klabu ambayo anataka kuitumikia Barani Afrika kwa sasa, basi ni Simba SC.

“Naipenda Simba kuliko kila kitu. Najua kuna watu wengi walifikilia kuwa mimi nitavaa rangi ya kinyoka nyoka. Kama kuna klabu Afrika nataka kucheza basi ni Simba Sports Club.” amesema Cesar Manzoki.

Msimu uliopita Manzoki alikuwa akiitumikia Vipers SC ya Uganda na baadae aliuzwa kwenye Klabu ya Dallian International ya China.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii